TRANSLATE THIS BLOG

Tuesday, April 7, 2015


TENGA AULA TENA CAF


MWENYEKITI wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Leodegar Tenga amerejea katika nafasi yake ya Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shiriksiho la Soka Afrika (CAF) baada ya uchaguzi uliokwenda sambamba na Mkutano Mkuu mjini Cairo, Misri Aprili 6 na 7 mwaka huu.

Tenga, Rais wa zamani wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), sasa ataitumikia nafasi hiyo kwa miaka mingine minne kama Mkuu wa ukanda wa CECAFA
(Rais wa FIFA Sepp Blatter akiwa na Leodegar Chilla Tenga walipokutana hivi karibuni makao makuu ya FIFA jijini Zurich)
Taarifa ya Katibu Mkuu wa CECAFA , Nicholas Musonye leo, imesema kwamba Mkutano Mkuu wa CAF ambao hufanyika kila mwaka, ulianza Jumatatu mjini Cairo na nchi zote 54 wanachama zikiwemo 12 za CECAFA zilihudhuria.

Wanachama wa CECAFA ni Burundi, Kenya, Uganda, Tanzania, Somalia, Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Zanzibar, Rwanda, Sudan na Sudan Kusini.

Tenga alichaguliwa bila kipingamizi, baada ya aliyekuwa mpinzani wake, Hassan Suleiman wa Djibouti kujitoa na kumsapoti Nahodha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars.



KUELEKEA DERBY  YA MANCHESTER.....
Man Utd v Man City: Ni muda muafaka kukutana , asema Vincent Kompany

 Vincent Kompany says it is a good time for Manchester City to play local rivals United, despite being overtaken by Louis van Gaal's side in the table.

City's recent record of three defeats in five games, coupled with United's five successive wins, has seen the champions slip from second to fourth.

Before Sunday's meeting, the City skipper said:  "It's a good moment to go into a derby.

LEO Mabingwa na Vinara wa Serie A huko Italy, Juventus, wana kibarua kigumu cha kugeuza kipigo walichopewa Nyumbani kwao na Fiorentina kwenye Nusu Fainali ya Coppa Italia.

Katika Mechi ya kwanza iliyochezwa huko Juventus Stadium, Fiorentina waliichapa Juve Bao 2-1 na Leo Fiorentina wako kwao Stadio Artemio Franchi kulinda ushindi huo ili watinge Fainali.

Mechi nyingine ya Marudiano ya Nusu Fainali itachezwa kesho Jumatapo huko Stadio San Paolo kati ya Napoli na Lazio ambazo zilitoka 1-1 katika Mechi ya kwanza.

Tayari Marefa wa Mechi hizi wameshatangazwa na Davide Massa atachezesha Fiorentina v Juventus na Daniele Orsato ile ya Napoli v Lazio.


Italy - Coppa Italia
April 7
21:45 Fiorentina ? - ? Juventus

kwa mechi za leo za ligi mbalimbali tembelea http://www.livescore.com/

DFB-POKAL: LEO DORTMUND KUWANIA KUINGIA NUSU FAINALI!

Klabu 7 za Bundesliga na moja ya Daraja la 3, Arminia Bielefeld, Leo na Jumatano zitawania Nafasi 4 za kuingia Nusu Fainali ya Kombe la Ujerumani, DFB-Pokal.

Miongoni mwa hizo 7 za Bundesliga, 4 zipo kwenye 4 Bora, na pia ipo Borussia Dortmund ambayo Msimu huu inasuasua na ipo Nafasi ya 10.

Kwa Dortmund, ambao Leo watacheza kwao Signal Iduna Park na Hoffenheim, hii ndio nafasi yao pekee iliyobaki Msimu huu kutwaa Taji na Kocha wao, Jurgen Klopp, amesisitiza hilo.

Mabingwa Watetezi wa DFB-Pokal Bayern Munich wana Mechi ngumu ya Ugenini Jumatano dhidi ya Timu iliyo Nafasi ya 4 kwenye Bundesliga, Bayer Leverkusen lakini hilo halikumkatisha tamaa Kiungo wao kutoka Spain, Xabi Alonso, ambae ameshawahi kutwaa Vikombe huko kwao Spain na England na safari hii anataka cha Nchini Germany ambacho kwa Bayern itakuwa DFB-Pokal yao ya 3 mfululizo.

Katika Mechi nyingine za Robo Fainali, Leo Wolfsburg watakuwa Wenyeji wa Freiburg wakati Arminia Bielefeld, Timu ya Daraja la 3 iliyozibwaga katika Raundi zilizopita Klabu za Bundesliga Hertha Berlin na Werder Bremen, itakuwa Nyumbani kucheza na Borussia Monchengladbach hapo Jumatano.

DFB-Pokal

Robo Fainali;Jumanne Aprili 7
20;00 Wolfsburg v SC Freiburg

21;30 Borussia Dortmund v Hoffenheim
Jumatano Aprili 8

20;00 Arminia Bielefeld v Borussia Mönchengladbach
 21;30 Bayer Leverkusen v Bayern Munich

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - RELEASE NO. 51

TAREHE 07 APRILI 2015

U-15 YAINGIA KAMBINI


Timu ya Taifa ya Tanzania ya Vijana wenye umri chini ya miaka 15 (U-15) imeingia kambini leo katika hoteli ya Itumbi iliyopo magomeni chini ya kocha mkuu Adolf Rishard kujiandaa na progamu ya vijana kuwania kufuzu kwa fainali za U-17 mwaka 2017 nchini Madagascar.
Akiongea na waadishi wa habari leo kwenye ukumbi wa habari wa TFF Karume, mwenyekiti wa kamati ya soka la vijana Bw. Ayoub Nyenzi amesema kamati yake imeandaa programu maalumu ya kuwaanda vijana kwa ajili ya kuichezea timu ya Taifa U-17 mwaka 2017.

TFF imeandaa program hiyo ya vijana U-15 ambao watakua kambini kwa muda siku 10, wakifanya mazoezi uwanja wa Karume na kucheza michezo kadhaa ya kirafiki na timu za Azam U17 na shule ya Sekondari Makongo.

Kocha mkuu na timu yake ya U-15 atazunguka mikoa saba nchini kwa ajili ya kucheza michezo kadhaa ya kirafiki na kungamua vipaji vingine kwa ajili ya kuboresha timu yake. Mikoa itayotembelewa ni Mbeya, Mwanza, Morogoro, Arusha, Tanga, na Dar es alaam (Ilala, Kinondoni, Temeke).

Aidha katika kuhakikisha timu hiyo inakua tayari kwa michuano ya kuwania kufuzu kwa fainali za U-17 mwaka 2017 nchini Madagascar, timu hiyo ya vijana itafanya ziara ya mafunzo mwezi Disemba mwaka huu katika nchi za Malawi, Zambia, Zimbambwe, Botswana na Afrika Kusini kwa kucheza michezo ya kirafiki.

Mwezi Februari 2016 timu hiyo itacheza michezo miwili ya kirafiki na timu za mikoa ya Dodoma na Mwanza, kabla ya kuelekea tena katika ziara kwenye nchi za Burundi, Rwanda, Uganda na Kenya mwezi Aprili 2016.

Ratiba ya CAF kuwania kufuzu kwa fainalizaAfrika 2017 inatarajiwa kuanza mwezi Juni 2016, ambapo kikosi cha Tanzania kitakua kimeshapata muda mzuri wa maandalizi kwa lengo la kuhakikisha timu inashiriki fainali hizo nchini Madagascar 2017.

Fainali za U-17 mwaka 2017 zinatarajiwa kufanyika nchini Madagascar, huku Tanzania ikitarajia kwa kuwa mwenyeji wa fainali hizo za vijana U-17 kwa mwaka 2019.

Jumla ya wachezaji 30 wameitwa kuingia kambini, wachezaji hao ni Kelvin Deogratius, Magazi Dotto, Anthon Shilole (Geita), Sadik Sud Ramadhani , Mwinchumu Yahya(Tanga),Faraji John, David Mbakazi , Juma Juma, Pius Raphael, Davison Meddy, Maulid Lembe (Dodoma), Ibrahim Koba (Morogoro).

Wengine ni Abubakar Badru Nassoro, Yusuf B.A. Khalfani, All Hafidh Mohamed (Kusini Pemba), Joachim Mwenda, Charles Cassiano, Luqman Shauri (Tanga), Juma Zuberi (Kigoma), Ismail Abdallah (Kusini Pemba), Robert Philipo (Arusha), Alex Peter, Mohamed Ally, Rashid Kilongola (Kinondoni), Saad Juma (Mkoa Magharibi), Ibrahim Shamba (Kusini Unguja), Ally Msengi, Klevin S.Kijili (Mwanza), Frank Abel (Simiyu) na Bryan Jamal.

VPL KUENDELEA KESHO


Ligi kuu ya Vodacom Tanzania inatarajiwa kuendelea kesho jumatano katika viwanja viwili jijini Dar es salaam, kwa vinara wa ligi hiyo Young Africans kuwakaribisha Coastal Union kwenye dimba la Uwanja wa Taifa.

Uwanja wa Chamazi Complex, wenyeji timu ya Azam FC wanaokamata nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu, watawakaribsiha wagonga nyundo kutoka jijini Mbeya timu ya Mbeya City FC.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Natasha Jonas retires: British Olympic boxer quits aged 30

 Natasha Jonas, the first woman to box for Great Britain at the Olympic Games, has retired 16 months before Rio 2016.

The Liverpudlian won bronze at the 2012 World Championships before reaching the quarter-finals at the London Olympics.

The 30-year-old, who hopes to move into coaching, told BBC Sport: "I don't think I've got the hunger and dedication to achieve any more.

"My mind is wandering to other things, and there's younger people coming through that want it a bit more."

Jonas took up boxing in 2005 to lose weight and rose through the amateur ranks before competing for Britain alongside gold medallist Nicola Adams and Savannah Marshall at London 2012.

Who is Natasha Jonas?

Date of birth: 18 June 1984
Height: 1.72m (5ft 7in)

Birthplace: Liverpool
Olympic division: Lightweight

Did you know? Jonas had to drop down two weight divisions (8kg) for the Olympics as there is no welterweight category.