TRANSLATE THIS BLOG
Monday, September 24, 2012
Gerrard: Maamuzi ya Referee yametugarimu!!!!!
Steven Gerrard Amesema maamuzi yaliyofanywa na referee
Mark Halsey baina yao na Man utd nyumbani Anfield jana
jumapili katika muendelezo wa ligi kuu ya soka uingereza ,
ilikuwa ni sababu ya Liverpool kupokea kichapo cha
2-1 kutoka kwa Manchester United
Jonjo Shelvey alitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumchezea vibaya Jonny Evans, ... United walishinda mechi hiyo kwa goli la pili lililotiwa kimiani na Robin van Persie spot kick.
kipigo hicho kwa Liverpool kimewafanya kuendelea kusalia na two points katika mechi tano walizokwisha cheza....
TERRY ABWAGA MANYANGA KUCHEZEA ENGLAND!!
LEO KUMKABILI PILATO wa FA kwa TUHUMA za UBAGUZI!!...........
John Terry, Nahodha wa Chelsea ambae ameichezea England mara 78, ametangaza kustaafu kuichezea Timu ya Taifa ya England huku leo akitakiwa kufika mbele ya Jopo la FA, Chama cha Soka England, akikabiliwa na tuhuma za kumkashifu kibaguzi Beki wa QPR Anton Ferdinand wakati wa Mechi ya Ligi Kuu England iliyochezwa Loftus Road Mwezi Oktoba Mwaka jana kati ya QPR na Chelsea.
Akitangaza kustaafu kwake kuichezea England, Terry alisema kuendelea kuichezea England huku FA imeamua kumshitaki wakati Mahakama imemsafisha kunamwia vigumu.
Mara baada ya tukio hilo la kutuhumiwa kukashifu kibaguzi, FA ilifungua uchunguzi lakini suala hilo likadakwa na Polisi na hatimae kutua Mahakamani baada ya Shabiki mmoja kulalamika lakini Terry alishinda Kesi hiyo Mwezi Julai.
Mara tu baada ya Kesi Mahakamani kumalizika, FA ilifungua tena uchunguzi wake na kuamua kumshitaki Terry na endapo atapatikana na hatia huenda akafungiwa kwa muda mrefu kama alivyofanyiwa Luis Suarez wa Liverpool baada ya kumkashifu kibaguzi Patrice Evra wa Manchester United.
John Terry, ambae alianza kuichezea Chelsea tangu ana Miaka 14, alianza kuichezea England Mwaka 2003 na kuteuliwa kuwa Kepteni wake Mwaka 2006 baada ya David Beckham kujiuzulu wadhifa huo.
Mwaka 2010, Terry alinyang’anywa Ukepteni na Meneja wa wakati huo Fabio Capello baada ya kuibuka skandali la kutembea na Bibi wa Mchezaji mwenzake wa Chelsea na England Wayne Bridge.
Lakini, baada ya kuumia aliekuwa Nahodha wa England Rio Ferdinand, Terry alipewa tena Ukepteni ambao alinyang’anywa na FA Februari Mwaka huu kufuatia kuamuliwa kupelekwa Mahakamani kwa tuhuma za kumkashifu kibaguzi Beki wa QPR Anton Ferdinand, kitendo ambacho pia kilimfanya
Tuesday, September 18, 2012
Wenger Hana uhakika na Walcott kubakia gunners !!!!!!!.........
Meneja wa washika bunduki wa london Arsenal mzee
Arsen Wenger ,amesema hana uhakika na mustakabali wa
baadae wa winga wake wa kingereza Theo kama atakubali
kusain mkataba mpya ......na amekubali kuwa jambo hilo
kunchanganya .....
Walcot alikuwa ndie aliyehitimisha idadi ya magoli katika ushindi wa bao
6-1 dhidi ya New Boys Southampton katika uwanja wa nyumbani
Emarate wikiend iliyopita katika muendelezo wa ligi kuu uingereza....
Haya yamejiri baada ya kuibuka tetesi kwamba katika wiki ya mwisho
kabla ya dirisha la usajili kufungwa Walcott alikataa mkataba mpya
ambao angekuwa akipokea 75,000 pounds kwa week and was instead,
holding out for 100,000.
Theo 23,amesalia na mwaka mmoja tu kuitumikia Arsenal.
UEFA CHAMPIONZ LIGI: Tathmini Mechi za leo Jumanne!
BIGI MECHI ni Santiago Bernabeu Real Madrid v Man City!!.....
Jumanne ya leo Septemba 18 ndio mwanzo rasmi wa Michuano
ya hatua ya Makundi ya UEFA ya kusaka Klabu Bingwa Ulaya,
UEFA CHAMPIONZ LIGI, na zitakuwepo Mechi 8 za Makundi A
hadi D lakini, bila shaka, kati ya hizo, BIGI MECHI, ile
Mechi ya Mvuto, ni ile itakayochezwa Uwanja wa Santiago
Bernabeu kati ya Mabingwa wa Spain Real Madrid na Mabingwa
wa England, Manchester City.
=====================
RATIBA:
[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, TANZANIA]
Jumanne Septemba 18
GNK Dinamo - FC Porto
Paris Saint-Germain FC - FC Dynamo Kyiv
Montpellier Hérault SC - Arsenal FC
Olympiacos FC - FC Schalke 04
Málaga CF - FC Zenit St. Petersburg
AC Milan - RSC Anderlecht
Borussia Dortmund - AFC Ajax
Real Madrid CF - Manchester City FC
=====================
TATHMINI MECHI ZA JUMANNE
KUNDI A
-GNK Dinamo Zagreb v FC Porto
-Paris Saint-Germain FC v FC Dynamo Kyiv
=====================
Klabu ‘Tajiri’ Paris Saint-Germain wanarejea tena kwenye
UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa mara ya kwanza tangu Msimu
wa 2004/5 na watakuwa wenyeji wa Dynamo Kiev
Uwanjani Parc des Princes.
PSG, chini ya Meneja Carlo Ancelotti, wameanza vyema
kwenye Ligi ya Ufaransa, Ligi 1, kwa kutoka sare Mechi 3 na
kushinda mbili huku Straika wao mkubwa Zlatan
Ibrahimovich akipiga bao 5.
Mbali ya Ibrahimovich, PSG wanao hatari nyingine kina
Javier Pastore na Ezequiel Lavezzi na pia kuanza tena
kucheza kwa Beki toka Brazil, Thiago Silva, ambae hajaichezea
Timu yake mpya baada ya kuumia akiwa na Brazil
kwenye Michezo ya Olimpiki, kutawaongezea nguvu.
Lakini Dynano Kiev sio nyanya na wameanza vyema
kwenye Ligi yao ya Ukraine kwa kupoteza Mechi mbili
tu kati ya 9 walizocheza huku tishio lao kubwa likitoka
kwa Mnigeria Ideye Brown ambae amewafungia
bao 8 Msimu huu.
Kwenye Kiungo, Dynamo Kiev wanae Mchezaji wa zamani
wa Tottenham Niko Kranjcar ambae kwenye Ligi ya
Ukraine amepachika bao 4.
Mechi nyingine ya Kundi A ni ile itayochezwa Stadion Maksimir
kati ya wenyeji Dinamo Zagreb na FC Porto.
Wakiwa bila ya Straika wao mahiri kutoka Brazil, Hulk, ambae
wamemuuza kwa Zenit St Petersburg, FC Porto
watawategemea Lucho Gonzalez na James Rodriguez
kuwapatia magoli.
Lakini Dinamo Zagreb, wakiwa na mashine yao ya Kibrazil
ya magoli, Sammir, hawajafungwa hata Mechi moja
kwenye Ligi yao Msimu huu, wapo kileleni, na
watataka kufuta uchungu wa Msimu uliopita ambao
kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI walifungwa Mechi zao
zote 6 za Kundi lao na kupachikwa jumla ya bao 22.
Moja ya vipigo hivyo 6 ni kile cha 7-1 mikononi
mwa Lyon na kuleta uzushi kuwa wamepanga matokeo.
KUNDI B
-Montpellier Hérault SC v Arsenal FC
-Olympiacos FC v FC Schalke 04
=====================
Straika wa Arsenal, Olivier Giroud, anarudi tena Klabu
yake ya zamani Montpellier ambayo ilimuuza kwa
Arsenal kabla Msimu huu kuanza huku akiwa bado
akisaka bao lake la kwanza kwa Klabu yake
mpya katika Mashindano rasmi.
Arsenal wanatinga kwenye Mechi hii ya Ulaya wakitoka
kuitandika Southampton bao 6-1 hapo juzi mechi
ambayo walicheza bila ya Giroud ingawa
Mchezaji wao mpya mwingine, Lukas Podolski, aling’ara.
Tofauti na Arsenal, Mabingwa wa Ufaransa
Montpellier wanatinga kwenye Mechi hii wakiwa
wanasuasua huko kwao kwenye Ligi 1 wakiwa
wameshinda Mechi moja tu kati ya 5 walizocheza
ikiwa ni pamoja na kichapo cha 3-1 mikononi
mwa Reims Ijumaa iliyopita.
Katika Mechi nyingine ya Kundi B, Schalke watakuwa
safarini kucheza Uwanja wa Karaiskakis nyumbani
kwa Mabingwa wa Ugiriki Olympiacos ambao
wameanza vyema kutetea Taji lao kwa
kushinda Mechi zao zote 3.
Tishio kubwa kwa Olympiacos ni toka kwa Schalke
ni lile la Straika wa Holland Klaas-Jan Huntelaar
ambae ni mfungaji hatari.
KUNDI C
-Málaga CF v FC Zenit St Petersburg
-AC Milan v RSC Anderlecht
=====================
AC Milan, walioanza vibaya kwenye Ligi yao ya Italy
Serie A na pia kuchapwa 1-0 hivi juzi na Atalanta,
wanawakaribisha Timu ngumu ya Anderlecht ya
Ubelgiji ambayo huko kwao haijafungwa katika Mechi 7.
Chini ya Kocha Massimiliano Allegri, AC Milan bado
inayumbishwa na kuondokewa kwa Nyota wao
kadhaa Msimu huu ambao ni Zlatan Ibrahimovic
na Thiago Motta waliokwenda Paris Saint-Germain
na wengine ni Wakongwe Alessandro Nesta,
Filippo Inzaghi, Gianluca Zambrotta, Gennaro Gattuso,
Mark van Bommel na Clarence Seedorf.
Pia AC Milan imempoteza Straika Antonio Cassano
ambae walibadilishana na yule wa Inter Milan
Giampaolo Pazzini lakini pia wameweza kununua
Wachezaji wawili, Kiungo Nigel de Jong
na Beki Francesco Acerbi.
Mechi nyingine ya Kundi C ni kati ya Timu mbili ambazo
zimeanza vizuri Ligi za nyumbani kwao ambazo ni
Malaga ya Spain na Zenit St Petersburg ya Urusi.
Ingawa Malaga wamempoteza Santi Cazorla
alieenda Arsenal lakini kwenye La Liga
wanafanya vyema na wako nafasi ya pili.
Zenit St Petersburg, chini ya Kocha Luciano Spalletti,
wanafanya vyema hasa ukuta wao imara na
Straika Alexander Kerzhakov amekuwa akifunga
bao zao nyingi kabla na kuimarishwa kwa
kuwanunua Hulk na Kiungo Axel Witsel.
KUNDI D
-Borussia Dortmund v AFC Ajax
-Real Madrid CF v Manchester City FC
=====================
Mechi ya Real Madrid na Manchester City Uwanjani
Santiago Bernabeu ndio gumzo la kila pembe Duniani.
Man City, chini ya Kocha Roberto Mancini, Msimu
uliokwisha walishindwa kuvuka hatua ya Makundi
ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na safari hii tena wako
kwenye ‘Kundi la Kifo’ ambalo pia wako Mabingwa
wa Ujerumani Borussia Dortmund na Mabingwa
wa Holland, Ajax Amsterdam.
Hii ndio Mechi ambayo, pengine, itathibitisha
kukomaa kwa Man City lakini pengine imekuja
kwao kwenye wakati mbaya kwani Real Madrid,
chini ya Kocha makeke Jose Mourinho, wako
kwenye wakati mgumu kwenye La Liga baada ya
kuanza utetezi mbovu wa Taji lao huko Spain.
Wakati Man City hawajafungwa kwenye Ligi Kuu
England wakiwa nafasi ya 4, Real Madrid wameshinda
Mechi moja tu na wapo nafasi ya 14 kwenye La Liga
huku wakigubikwa na utata kuhusu hatima ya Staa
wao mkubwa Cristiano Ronaldo ambae amebainisha
hana furaha Klabuni hapo.
Hii ni Mechi ambayo Mourinho lazima ashinde ili kurekebisha
Jahazi lake linaloenda mrama na hilo, pengine, linaweza
kuashiria maafa kwa Man City.
Mechi nyingine ya Kundi D ni ile itakayochezwa
Westfalenstadion, Uwanja ambao unasifika kwa
kelele, pale Ajax Amsterdam watakapotua kuwavaa
wenyeji Borussia Dortmund.
Baada ya kumpoteza Shinji Kagawa aliehamia Manchester
United, Dortmund walimnunua Marco Reus toka
Borussia Moenchengladbach na amekuwa moto.
Lakini Ajax, chini ya Staa wa zamani wa Holland Frank de Boer
, si mzaha na Msimu huu hawajapoteza Mechi.
Ajax, licha ya kuwapoteza Wachezaji wao Jan Vertonghen
(aliekwenda Tottenham), Gregory van der Wiel (Paris Saint-Germain)
na Vurnon Anita (Newcastle United), bado wanao
wengine tishio kina Thulani Serero, Tobias Sana na Siem de Jong.
RATIBA:
[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, Bongo Taimu]
Jumatano Septemba 19
FC Shakhtar Donetsk - FC Nordsjælland
Chelsea FC - Juventus
LOSC Lille - FC BATE Borisov
FC Bayern München - Valencia CF
FC Barcelona - FC Spartak Moskva
Celtic FC - SL Benfica
Manchester United FC - Galatasaray A.S.
SC Braga - CFR 1907 Clu
Monday, September 10, 2012
Rossi wants to work with Zeman
Giuseppe Rossi's agent has said the striker "would love to work" with Roma boss Zdenek Zeman, with a January switch for the player appearing likely.
GettyImages
Giuseppe Rossi: Set to leave Spain?
Rossi, who has been linked with numerous clubs across Europe, remained with relegated Villarreal after undergoing a second major knee operation which is expected to keep him out of action until at least March.
The 25-year-old former Manchester United man has yet to play a single minute since suffering his original injury in October 2011 but his agent, Federico Pastorello, has given the Serie A club, and their boss, a glowing reference, while also revealing a previous deal with the club nearly went through.....passionfleva@rocketmail.com
Del Bosque: kombe la Dunia 2014 limeanza kwa Spain
Bosi wa timu ya taifa ya spain ambae ndie bingwa wa dunia amesema wao wanaanza sasa harakati zimeanza kwaajili ya kujikakikishia wanapata ticket kwa ajilili ya World Cup mapema.
BINGWA MTETEZI SPAIN YUPO KUNDI I PAMOJA NA TIMU ZA France, Finland, Georgia NA Belarus ,KOCHA WA TIMU HIYO Del Bosque ANAMATUMAINI YA KUFANYA VIZURI KATIKA HATUA HII NA HAPO KESHO SHUGHULI INAANZA RASMI
"KOMBE LA DUNIA HALIANZI 2014,NI SASA DHIDI YA Georgia in Tbilisi," Del Bosque told AS. "NA ILI SPAIN WAENDELEE KUTETEA TAJI LAO NILAZIMA WAWE NA UBORA KWANZA KWA BRAZIL
Spain WANAINGIA UWANJANI KESHO KWA KUJIAMINI ZAIDI BAADA YA IJUMAA KUTOA KIPIGO CHA MBWA MWIZI KWA WARABU WA SAUDI ARABIA CHA BAO 5-0
Di Stefano: Pele Bora zaidi....
Legendary Real Madrid forward Alfredo Di Stefano anaamini kwamba mkongwe katika soka Pele alikuwa ni bora kuliko Lionel Messi Cristiano Ronaldo.
Di Stefano: Pele is better than Lionel Messi
Di Stefano kwa sasa anaumri wa miaka 86,amemsifia pele na kusema yeye alikuwa mkali kuliko ubora waliokuwa nao vijana hawa wa siku hizi japokuwa nao ni bora.
"amesema pele ni mchezaji bora ambae hakuna tena atakaetokea kama yeye .... Messi na Cristiano Ronaldo wote na bora lakini Pele alikuwa zaidi ," Di Stefano told El Colombiano.
Mu Argentine akaamua kuzungumzia tofauti za nyota hao wanaopatikana La Liga stars.
"Messi is the more technical player of the two. He's better inside the area, the way he handles the ball and dribbles. You can see that he enjoys himself playing," Di Stefano said.
"Cristiano has a better body and is physically very strong. He has pace, speed and is a player with courage, and he can use both feet."
Di Stefano zaidi ya mechi 300 Real Madrid, na kufanikiwa kushinda makombe nane ya ubingwa wa spain (La Liga)na five European Cups.
MIMI NDIO No. 1 WA SPURS
Mlinda mlango wa Tottenham mwenye umri wa miaka 41 anaamini yeye ataendelea kuwa namba 1 wa spurs licha ya kukabiliana na ushindani kutoka kwa goalkeeper wa kifaransa aliyesajiliwa toka Lyon
"Right now I believe the shirt is mine to lose, I believe the manager came out and said that. If that's the case then great," he told Sky Sports.
Raheem Sterling, Livermore na Lallana wachukuliwa England!!
Kocha wa England Roy Hodgson amelazimika kumchukua kinda wa Liverpool Raheem Sterling, Chipukizi wa Tottenham Hotspur Jake Livermore na yule wa Southampton Adam Lallana ili kuongeza nguvu Kikosi chake kwa ajili ya Mechi ya Kundi H ya Kombe la Dunia dhidi ya Ukraine itakayochezwa Jumanne Usiku Uwanjani Wembley baada ya Kikosi chake kukumbwa na upungufu kufuatia Theo Walcott kuondoka baada ya kuugua.
Mbali ya Walcott, Straika wa Chelsea, Daniel Sturridge, nae anaugua na huenda asiwepo hiyo Jumanne.
Walcott amekuwa Mchezaji wa 5 kuondoka kwenye Kikosi cha sasa cha England na wengine ni majeruhi John Terry, Ashley Cole, Adam Johnson na Andy Carroll na kuifanya Timu ibakiwe na Wachezaji 18 tu.
Upungufu huu, hasa kuondoka kwa Walcott na kuugua kwa Sturridge, kumemfanya Kocha Hodgson aite Chipukizi kuimarisha Kikosi.
Uteuzi wa kushangaza wa Hodgson ni kumwita Winga Raheem Sterling wa Liverpool [Pichani], mwenye Miaka 17 tu, ambae ameichezea Liverpool Mechi 5 tu.
Hata hivyo Sterling, Mzaliwa wa Jamaica, amewahi kuchezea Timu za Vijana za England za U-17 na U-19.
Jake Livermore wa Tottenham, mwenye Miaka 22, amewahi kuichezea England Mechi moja alipotokea benchi na kucheza na Italy kwenye Mechi ya Kirafiki Mwezi uliopita.
Winga Lallana, Miaka 24, amewahi kuichezea mara moja tu Timu ya Vijana ya England ya U-21 na hii ni mara ya kwanza kuitwa kwenye Kikosi cha Kwanza.
Akiongelea uteuzi wake huu, Hodgson amesema: “Hii ni nafasi nzuri kuwaita Wachezaji Vijana waje kuona mambo. Bado tunao Wachezaji wa kutosha kukabili upungufu kwa Mechi na Ukraine lakini vyema pia ukawa na hawa Vijana!”
Pengine tatizo kubwa kwa Hodgson ni kuamua nani atachukua nafasi ya John Terry kwenye Sentahafu kati ya Gary Cahill na Phil Jagielka.
WAKUFUNZI WA WAAMUZI WA FIFA WAMEANZA KUNOLEWA
KOZI ya wakufunzi wa waamuzi (Futuro III Refereeing Course) ya Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA) Imeanza leo kwenye hoteli ya Holiday Inn jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) Boniface Wambura, kozi hiyo imeanza saa tatu asubuhi imeshirikisha jumla ya washiriki 69 kutoka nchi 21 za Afrika.
Amesema kozi hiyo inayotarajiwa kumalizika Septemba 22 mwaka huu inafanyika katika maeneo mawili ya ufundi (technical) na utimamu wa mwili (fitness).
Nchi washiriki ni Afrika Kusini, Botswana, Eritrea, Ethiopia, Gambia, Ghana, Kenya, Lesotho, Liberia, Malawi, Mauritius, Namibia, Nigeria, Seychelles, Sierra Leone, Somalia, Swaziland, Tanzania, Uganda, Zambia na Zimbabwe.
“Washiriki kutoka Tanzania kwenye kozi hiyo ni Joan Minja, Leslie Liunda na Soud Abdi (technical) na Riziki Majalla (fitness),”.
Wambura amesema baadhi ya wakufunzi wa kozi hiyo wanaotoka FIFA na Shirikisho la soka Afrika (CAF) ni Carlos Henriques anatoka Afrika Kusini, Fernando Gracia (Hispania), Steve Bennett (Uingereza), Tarek Bouchamaoui (Tunisia), James Sekajugo (Uganda), Bester Kalombo (Malawi), Felix Tangawarima (Zimbabwe) na An-Yan Lim Kee Chong (Mauritius).
Aidha, Wambura amesema kozi hiyo imefunguliwa na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya CAF na mjumbe wa Kamati ya Vyama (Associations Committee) ya FIFA.
VITALI KLITSCHKO AMTWANGA MANUEL CHARR WA UJERUMANI
Bondia Manuel Charr wa Ujerumani akiokolewa na mwamuzi baada ya kupigwa na Vitali Klitschko na kuchanika jichoni na kutokwa damu nyingi kama anavyoonekana.
MOSCOW, Russia
Manuel Charr, ambaye alshinda katika raundi kama hiyo alipoumana na Danny Williams, juzi alilazimika kutoendelea na pambano lake dhidi ya Vitali, kutokana na konde zito lililomchana juu ya jicho lake la kulia
BINGWA wa WBC Vitali Klitschko, alifanya kazi rahisi ulingoni kumuwezesha kuibuka na ushindi pasipo changamoto kubwa kutoka kwa Mjerumani Manuel Charr, katika dakika ya mwisho ya raundi ya nne jijiji hapa.
Klitschko, 41, ameibuka mbabe wa pambano hilo dhidi ya mpinzani wake ambaye hakuwahi kupigwa huko nyuma.
Charr, ambaye alipata ushindi wa raundi kama hiyo alipoumana na Mwingereza Danny Williams, alilazimika kutoendelea na pambano hilo kuokana na konde zito lililomchana juu ya jicho lake la kulia na kumsababishia kumwagika kwa damu nyingi.
Hata hivyo Charr alikuja juu kupinga maamuzi – kufuatia majibu ya uchunguzi wa madaktari kuwa alikatwa na kitu na kwamba jeraha lake halikutokana na ngumi, hivyo kupinga matokeo.
Klitschko kwa mara nyingine anaingia katika ushindi wa utata, baada ya Februari mwaka huu kumchapa Dereck Chisora kwa pointi, na kusababisha mgogoro baina yam kali huyo na David Haye wakati wa mkutano na vyombo vya habari.
Haye, ambaye alipigwa kwa pointi na ndugu wa kuzaliwa wa Vitali, Wladimir mwaka jana, alifanikiwa kumchapa Chisora KO Julai mwaka huu nma kuamua kuomba pambano dhidi ya mkongwe huyu Vitali.
Pambano baina ya Haye na Vitali, linaweza tu kufanyika kama raia huyo wa Ukraine atashindwa uchaguzi wa nchi yake ambako anawania ubunge, ambapo kama akishinda atalazimika kustaafu masumbwi.
Timu za Simba na Azam zimeandika barua Shirikisho la Soka nchini (TFF) kuomba mchezo wao wa kesho wa Ngao ya Jamii uchezwe usiku. Mchezo huo umepangwa kuanza saa kumi alasiri, lakini zenyewe zinataka uanze saa 12 jioni ama saa moja usiku.
Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’, alisema jana kuwa walikaa pamoja na Azam kuomba TFF wabadili muda wa kuanza pambano hilo hadi saa 12 jioni.
“Tulikaa na Azam tukaandika barua ya kuwaomba TFF wasogeze mbele muda wa kuanza mchezo huo, maana saa 10 watu wengi wanakuwa bado wako makazini,”alisema Kaburu. Mchezo wa Ngao ya Jamii ni ishara ya ufunguzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza Jumamosi ijayo.
Friday, September 7, 2012
Kevin Kimani @ SS com
Kevin Kimani @ SS com |
Kevin Kimani ajiunga Bocholter VV
winga wa zamani Mathare United Kevin Kimani amepata klabu mpya
.Kevin Kimani amejiunga na BOCHLTER VV ya ubeligiji kwa mkataba wa mwaka mmoja siku ya jumatano baada ya kutokuwa na klabu kwa miezi kadhaa...
his comes after his deal with German Division II side Aachen fell through following relegation to the lower league where non EU players can’t feature, he was rendered clubless.
“I have joined Bocholter VV and I hope to find back my form as I adapt to the European kind of football The club plays in division III side and this is the reason why I joined them so that I can be able to grow as I have a higher chance of being in the starting line-up.”
“My fans should rest assured that I will do my best to be where they want me to be. It is a long journey and this is just one of the step. The facilities here are superb and so far I have adapted well,” Kimani told supersport.com.
Kimani alikuwa mchezaji bora msimu uliopita baada ya kuewa kinara katika ufungaji Mathare United as the slum boys survived relegation. lakini pia alipigiwa kura kama kiungo bora wa mwaka.
He could make his debut during Belgian Super Cup against Gent.
HABARI FUPI FUPI
Beki wa Chelsea timu ya taiga ya uingereza Ashley Cole, 31, anajipanga kuondoka klabuni hapo mwezi wa kwanza au mwishoni maw msimu huu na kuelekea ufaransa katika klabu ya Paris Saint-Germain .
-------------------------------------------------------------------------------------------------------
meneja wa Real Madrid Jose Mourinho anaamini history pekee ya klabu hiyo itatosha kumbakiza nyota wa kireno Cristiano Ronaldo, 27,na kuwa out of Manchester City's reach.
--------------------------------------------------------------------------------------
Bosi wa washika bunduki wa london Arsenal mzee Arsene Wenger anamtaka beki wake Bacary Sagna, 29, na Kieran Gibbs, 22,kusaini mkataba mpya . Sagna atapewa of a nzuri japokuwa akishangazwa na sera za usajili klabuni hapo.
---------------------------------------------------------------------------------------
mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia, Radamel Falcao, 26, amekanusha taarifa zilizosema ataondoka Atletico Madrid na kuelekea katika ligi kuu uingereza na kujiunga na Manchester City au Chelsea.
-----------------------------------------------------------------------------------
kiungo wa QPR Samba Diakite amerejea nyumbani ufaransa kwa aajili ya matibabu zaidi. mchezaji huyo mwenye miaka 23 atapewa muda zaidi mpaka atakapo pona na kurejea katika hali yake ya kawaida.
-------------------------------------------------------------------------------------
meneja wa Newcastle United Alan Pardew anasubiria taarifa kamili juu ya Fabricio Coloccini baada ya beki huyo kuumia nyama za paja wakati akitumikia timu yake ya taifa Argentina.
KALI YA LEO: NAHODHA WA MANCHESTER UNITED AKAMATWA KWA KUFANYA MAPENZI HADHARANI
Star anayechipukia wa klabu ya Manchester United ya Uingereza amekamatwa na polisi kwa tuhuma za kuonekana akifanya tendo la ndoa na mpenzi wake hadharani.
Luke McCullough, 18, ambaye msimu uliopita alikuwa nahodha wa Academy ya United, alionekana kwenye kamera za CCTV akiwa na mwanamke wakifanya mapenzi saa 11 asubuhi baada ya kukesha usiku mzima klabu.
Mchezaji huyo raia wa Ireland amekuwa akitajwa na mabosi wa Old Trafford kama Jonny Evans mpya.
Tukio hilo lilotokea eneo la Concert Square, kwenye bar maarufu katika wilaya ya Liverpool, litamuudhi sana kocha wake Sir Alex Ferguson.
Fergie huwa na mkali sana kwa vijana wake hasa wachanga, na wiki iliyopita aliwakataza wachezaji wadogo wote chini ya umri wa miaka 23 kuendesha magari ya kifahari yanayogawiwa na mdhamani mpya wa klabu Chevrolet.
Imetaarifiwa kwamba Luke akiwa na demu wake walionekana wakiwa wapo nusu uchi huku wakifanya mapenzi, na ndipo polisi wakaenda eneo la tukio na kuwakamata.
Wapenzi hao walishatuliwa na polisi na kuonywa kisha wakaachiwa, na walipoondoka na kufika mbele kidogo wakarudia tena mchezo wao, polisi wanasema.
Maofisa wa polisi walienda tena mpaka kwenye eneo lile na kuwakamata kisha kuwapeleka kituoni na sasa wanakabiliwa na kesi ya kufanya mapenzi hadharani.
We are out for revenge, says Barcelona star Lionel Messi
The 25-year-old Argentine has warned that the Catalan giants are looking for a clean sweep of trophies this season
Lionel Messi says that Barcelona are relishing the challenge of competing on all fronts this season, while bemoaning their failure to land either La Liga or the Champions League last term.
Barca appeared on course to retain both trophies as the previous campaign drew to a close, before being knocked out of Europe's premier club competition by Chelsea in the semi-finals and losing their domestic crown to Real Madrid.
"Obviously I would have liked to win the Champions League and as always win everything," said Messi.
"Not beating Chelsea and reaching the final was painful for us, and for me especially having missed a penalty. But this year we will go for it all again, we are prepared."
The Argentine went on to say that although new coach Tito Vilanova has a different personality than Guardiola, his approach to football is the same.
"They are different personalities, but the philosophy is identical. The same people are working with Tito. Everyone has their own way of seeing things, to transmit. And yes they are different," he concluded.
BPL: Yatafakari kubana Mishahara Mikubwa Wachezaji, Matumizi kwa Klabu!
Msimu ujao, wa Mwaka 2013/14, UEFA inaanza rasmi kutumia zile Sheria zake mpya za kila Klabu kuishi kwa Mapato na Matumizi yake ya Mwaka wa Fedha husika, na Wasimamizi wa Ligi Kuu England wamekutana na kupendekeza Mishahara ya Wachezaji pamoja na Bajeti za Klabu zifuate mfumo mpya wa UEFA.
Klabu za England zinategemea mapato yao kuongezeka maradufu baada ya Makataba mpya wa TV kwa Kipindi cha 2013/16 kusainiwa hivi karibuni.
Wakati Manchester United na Arsenal zinataka Klabu za England zikubaliane tangu sasa na Sheria mpya za UEFA za kuzuia Mishahara mikubwa kwa Wachezaji na Klabu kujiendesha yenyewe kwa Mapato yake, zipo Klabu nyingi haziafiki hayo.
Kwa mujibu wa taratibu za FA, lazima Klabu 14 ziafike kati ya 20 ili Sheria ibadilishwe.
Ukiziondoa Klabu Tajiri Chelsea na Manchester City, Klabu nyingine ambazo hazijiafiki msimamo huu mpya ni Fulham, Everton, West Bromwich Albion, Newcastle na Tottenham Hotspur.
Klabu ambazo zimesimama kidete Sheria hii mpya ifuatwe ni West Ham, ambayo Mwenyekiti wake David Gold anataka kuwepo na kima maalum ya kiwango cha juu cha Mishahara ya Wachezaji.
David Gold yuko msimamo mmoja na David Whelan wa Wigan.
Peter Coates, Mmiliki wa Stoke City, amesema: “Nategemea tumekubaliana. Haiwezekani Fedha zote hizi ziwe za Wachezaji tu.”
Klabu zote 20 zimefikia maafikiano ya kuweka Makundi mawili ya Timu 10 kila moja ambayo yatatoa Ripoti zao mwishoni mwa Desemba ili uamuzi utoke.
BREAKING NEWS: Redknapp kocha mpya Bournemouth
Redknapp mwenye 65-year-old alikuwa hana timu baada ya kutimuliwa na timu ya london kaskazini ya Tottenham msimu uliopita na sasa amerejea katika soka baada ya kupata nafasi ya kuifundisha moja ya timu inayoshiriki League One side
Getty
Bournemouth ni klabu yenye maskani yake Goldsands Stadium ni timu Redknapp kabla yakutua spurs alikwishawahi kuitumikia klabu hiyo kama mchezaji na kuwa meneja katika kipindi cha nyuma....
mwenyekiti wa klabu Eddie Mitchell told the club's official website.
“bado anamapenzi na klabu na soka kwa ujumla
Redknapp aliitumikia kwa miaka minne klabu hiyo ya south coast side kama mchezaji na baadae kujiunga na West Ham mwaka 1972 na kucheza zaidi ya mechi 100 .
Harry alirejea kama manager mwaka 1983 na kuiletea mafanikio makubwa Football League Trophy and promotion from the Third Division.
TOKA TFF: TAIFA STARS v UGANDA CHAN 2014
Release No. 142
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Septemba 7, 2012
MECHI YA NGAO YA JAMII KUCHANGIA HOSPITALI YA TEMEKE
Asilimia tano ya mapato yatakayopatikana kwenye mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kati ya Simba na Azam yatakwenda kwenye Hospitali ya Temeke mkoani Dar es Salaam.
Kabla ya kukabidhi, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litakutana na uongozi wa Hospitali ya Temeke kupanga maeneo ambayo fedha hizo zitatumika kwenye hospitali hiyo.
Mechi hiyo ya uzinduzi rasmi wa msimu wa 2012/2013 itafanyika Jumanne ya Septemba 11 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Viingilio kwenye mchezo huo vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 kwa viti vya VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000.
WACHEZAJI WAWILI WAOMBEWA ITC URENO
Shirikisho la Mpira wa Miguu la Ureno (FPF) limetuma maombi Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupatia Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa wachezaji wawili waliokuwa wakicheza mpira nchini.
Wachezaji wanaoombewa ITC ni Hamis Thabit Mohamed (19) ambaye klabu yake ya mwisho aliyoichezea nchini ilikuwa African Lyon wakati mwingine ni Abuu Ubwa Zuberi (20) ambaye msimu uliopita alikuwa akiichezea timu ya Yanga.
Kwa mujibu wa FPF, wote wawili wanaoombewa ITC kama wachezaji wa ridhaa (amateur) ili waweze kujiunga na timu ya Atletico Sport Clube ya Ureno ambayo hata hivyo haikuelezwa iko daraja gani nchini humo.
Pia FPF imeombwa kupatiwa hati ya maelezo ya mchezaji (player’s passport) kwa kila mmoja ikiwemo taarifa za ushiriki wao katika mechi rasmi zinazotambuliwa na TFF wakiwa katika klabu zao hizo za zamani.
STARS YAPANGIWA UGANDA CHAN 2014
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imepangiwa kucheza na Uganda (The Cranes) katika raundi ya kwanza ya michuano ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zitakazofanyika Afrika Kusini mwaka 2014.
Kwa mujibu wa ratiba iliyopangwa jana (Septemba 7 mwaka huu) makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) jijini Cairo, Tanzania imeingia moja kwa moja raundi ya kwanza ambapo itacheza na Uganda.
Mechi ya kwanza itachezwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam kati ya Juni 21,22 na 23, 2013 wakati ya marudiano itakuwa Uwanja wa Mandela ulioko Namboole jijini Kampala kati ya Julai 5,6 na 7, 2013.
Nchi 38 zinashiriki katika mechi hizo za mchujo ambapo nyingine zitaanzia raundi ya awali itakayochezwa kati ya Novemba 30 na Desemba 1 na 2 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitakuwa kati ya Desemba 14,15 na 16 mwaka huu.
Ratiba imepangwa kwa makundi ya kanda ambapo jumla ya timu 16 ndizo zitakazocheza fainali hizo nchini Afrika Kusini. Kanda hizo ni Kaskazini itakayopeleka timu mbili katika fainali, Magharibi A (timu mbili), Magharibi B (timu tatu), Kati (timu tatu), Kati Mashariki (timu tatu), Kusini (timu tatu akiwemo mwenyeji Afrika Kusini).
Kwa upande wa kanda ya Tanzania (Kati Mashariki), timu zinazoanzia raundi ya awali ni Burundi, Eritrea, Ethiopia na Kenya.
Fainali za Kwanza za CHAN zilifanyika mwaka 2009 nchini Ivory Coast ambapo Tanzania ilishiriki huku Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) ikiibuka bingwa. Fainali za Pili zilichezwa mwaka 2011 nchini Sudan ambapo Tunisia ilitwaa ubingwa. Fainali za Kwanza zilishirikisha timu nane kabla ya kuongezwa hadi 16 za sasa.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Viwango vya hali ya juu vilivyoonyeshwa na chipukizi wa Yanga, Simon Msuva na Frank Domayo vimewaweka pabaya wakongwe Nizar Khalfan na Juma Seif ‘Kijiko’.
Kocha wa Yanga, Tom Saintfiet alisema jana amekuwa akifurahishwa na viwango ambavyo vimekuwa vikionyeshwa na chipukizi hao tangu walipojiunga na timu hiyo.
Mbelgiji huyo alisema,“nimekuwa nikimuanzisha Msuva badala ya Nizar nikiwa na lengo la kumjenga na kumpa uzoefu zaidi. Ni mchezaji anayekuja vizuri. Nafikiri atakuwa tegemeo kwa siku za baadaye.
” Msuva amecheza mechi zote tano za Yanga za kujipima ubavu kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu na kupachika mabao mawili dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda na African Lyon, pia alitoa pasi ya bao lililofungwa na Said Bahanunzi dhidi ya Coastal Union wakati Yanga ikishinda 2-1.
Domayo alitua Yanga akitokea JKT Ruvu ya Pwani na mpaka ameonyesha uwezo mkubwa hata kumfanya Kijiko aliyetamba na klabu hiyo msimu uliopita kuwa chaguo la tatu.
Domayo amekuwa akiingizwa kipindi cha pili katika kikosi cha Yanga na kuonyesha kiwango kizuri.
wakati huo huo NIYONZIMA mbioni Kuachana na YANGA
Kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Niyonzima amesema anatarajia kuachana na mabingwa wa Kombe la Kagame, Yanga mwishoni mwa msimu huu.
Akizungumza na gazeti la New Times la Rwanda, Niyonzima alisema anatarajia kwenda kucheza soka la kulipwa Ulaya, lakini kwa sasa anasubiri mkataba wake na Yanga umalizike mwezi Mei ili aondoke.
“Meneja wangu amekuwa akihangaika kunitafutia timu Ulaya. Tumekuwa na mawasiliano na klabu za ligi daraja la pili Hispania na Ligi Daraja la kwanza Ubelgiji.
“Kama mambo yakienda vizuri wakati wowote naweza kwenda kujiunga na timu hiyo (hakutaja jina la timu), kwa sababu mkataba wangu na Yanga unaniruhusu kuondoka kama nikipata klabu kubwa zaidi,” aliongeza Niyonzima.
Subscribe to:
Posts (Atom)