Saunders;Kocha mpya Wolves
Klabu ya Wolves imethibitisha kwamba Dean Saunders ndie meneja mpya wa timu hiyo hii nikufuatia kutimuliwa kwa aliekuwa kocha wa Wolves Stale Solbakken kutimuliwa siku ya jumamosi.
Saunders, 48, ameiwezesha Doncaster Rovers kusalia nafasi ya pili katika League One msimu huu na alianza kazi ya kuwa meneja akiwa na timu ya Wrexham.
Taarifa kutoka ndani ya klabu kupitia tovuti yao imesema: "Wolves wanapenda kuwafahamisha kwamba Dean Saunders ndie atakuwa meneja mpya . Doncaster Rovers wamekubali kumuachia kocha huyo mwenye umri wa miaka 48 kuelekea Molineux kufuatiwa kutimuliwa kwa aliyekuwa mwalimu wa timu hiyo Stale Solbakken siku ya jumamosi."
Saunders ni boss wa nne wa Wolves katika kipindi kisichopungua mwaka mmoja hii ni baada ya mwezi wa pili kutimuliwa kwa Mick McCarthy na kufuatiwa na and the Terry Connor.
No comments:
Post a Comment