Timu ya Taifa ya Tanzania itaondoka Mwanza Jumatano kwenda
Kampala, Uganda kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la CHAN
itakayochezwa Jumamosi katika Uwanja wa Mandela kuanzia saa kumi kamili
jioni.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini
jijini Mwanza chini ya Kocha Kim Poulsen tangu Julai 14 mwaka huu
kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili
itacheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
Timu hiyo itaondoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza saa 7.25 mchana kwa
ndege ya PrecisionAir, na inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
wa Entebbe saa 10.15 jioni.
Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya kikosi chake Jumanne.
No comments:
Post a Comment