TRANSLATE THIS BLOG

Wednesday, November 14, 2012


Pele apata nafuu baada ya kufanyiwa upasuaji wa nyonga.


Nyota wa zamani wa klabu ya Santos na timu ya taifa ya Brazil ambaye pia ni alama muhimu katika ulimwengu wa soka Edison Arantes do Nascimento ‘Pele’ amefanyiwa upasuaji wa nyonga na inaarifiwa ya kwamba anaendelea vizuri baada ya kuwa katika uangalizi mzuri mjini Sao Paulo.

Pele ambaye kwasasa ana umri wa miaka 72, alifanyiwa upasuaji huo katika hospitali ya Albert Einstein licha ya kwamba hakuna habari zaidi zilizo tolewa ikiwa ni agizo kutoka kwa familia ya gwiji huyo wa soka wa zamani.

Msemaji wake Jose Fornos ameidokeza Agence France-Presse akisema;
"kila kitu kimekwenda vizuri na ulikuwa ni upasuaji mdogo" 

Pele anaangaliwa kama ni mchezaji mkubwa kuwahi kutokea duniani akifunga magoli 1,300 na kushinda mataji matatu ya kombe la dunia katika miaka ya 1958, 1962 na 1970 katika cha uchezaji wake ulio tukuka.

Baada ya kuendelea kushikilia rekodi nyingi za dunia katika soka, hatimaye Pele wiki iliyopita alishuhudia moja ya rekodi yake ikivunjwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina na klabu ya Barcelona Lionel Messi ya kufunga magoli 75 katika kipindi cha mwaka mmoja

No comments:

Post a Comment