Habari Mpya
- Malawi na Tanzania kukutana leo kujadili mzozo wa mpaka
- Matukio ya hivi karibuni nchini Syria
- Kuendelea maandamano katika utawala wa Kizayuni wa Israel
- Al Ghanushi: Allah ataikomboa Palestina na Quds
- Wasaudia waendelea na maandamano nchini humo
- Makumi ya magaidi wauawa nchini Syria
- Bunge la Somalia kumchagua Rais leo
- Jumuiya ya EAC yaazimia kukabiliana na uhalifu
- Vikosi vya ulinzi vya vitakabiliana na chokochoko za maadui
- SADC yataka kuhitimishwa hitilafu za Congo na Rwanda
Jumatatu, 20 Agosti 2012 13:52
Malawi na Tanzania kukutana leo kujadili mzozo wa mpaka
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania na Malawi wanakutana leo katika
mji wa Mzuzu, ulioko kaskazini mwa Malawi kwa shabaha ya kujadiliana
juu ya mzozo wa nusu karne wa mpaka baina ya nchi mbili hizo.
Hivi
karibuni Tanzania na Malawi zilitumbukia katika malumbano makubwa ya
mpaka ambayo yalikaribia kuzitumbukiza nchi hizo katika vita.
Hata hivyo
mazungumzo ya hivi karibuni baina ya Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania na
Bi Joyce Banda wa Malawi huko Maputo Msumbiji yalipunguza kidogo
hitilafu hizo baada ya viongozi hao kusisitiza juu ya kutatuliwa
hitilafu hizo kwa njia za kidiplomasia.
Mgogoro huo, unalihusu Ziwa Nyasa, ambalo linatambulika nchini Malawi
kwa jina la Ziwa Malawi na ambalo tayari serikali ya Lilongwe imeshatoa
leseni za utafutaji mafuta kwa kampuni moja ya Uingereza.
No comments:
Post a Comment