TRANSLATE THIS BLOG

Monday, August 20, 2012

leo katika historia!!!!!!!!!!!Agosti 20


Leo ni Jumatatu tarehe Pili Mfunguo Mosi Shawaal mwaka 1433 Hijiria inayosadifiana na tarehe 20 Agosti mwaka 2012 Miladia Siku kama ya leo miaka 14 iliyopita, yaani Agosti 20 mwaka 1998 Marekani ilizishambulia kwa makombora Sudan na Afghanistan. Serikali ya Washington ilidai kwamba, watu walioshiriki katika kulipua kwa mabomu balozi za Marekani mjini Dar es Salaam Tanzania na Nairobi Kenya wiki mbili kabla, walikuwa na uhusiano na nchi hizo. Aidha Washington ilisema ilikishambulia kwa mabomu kiwanda cha kuzalisha madawa cha ash-Shifaa nchini Sudan kwa madai kwamba kilikuwa kikitengeneza mada za kemikali. Hata hivyo weledi wa masuala ya kisiasa walisema kwamba, sababu ya Marekani kufanya mashambulio ya mabomu dhidi ya Sudan na Afghanistan ilikuwa ni kujaribu kufunika fedheha ya kimaadili iliyokuwa ikimkabili rais wa nchi hiyo Bill Clinton. Kwa ajili hiyo mashambulizi hayo yaliamsha hasira za fikra za walio wengi na serikali nyingi duniani dhidi ya siasa za kutumia mabavu na kujichukulia maamuzi ya upande mmoja za Marekani. Siku kama ya leo miaka 849 iliyopita muwafaka na tarehe Pili Shawwal mwaka 584 Hijiria, alifariki dunia Ibun Ta'awidhi mshairi na mwanafasihi wa Baghdad. Alizaliwa mwaka 519 Hijiria na ujanani mwake aliwahi kufanya kazi mahakamani. Mshairi huyo wa Kiislamu alipitisha wakati wake mwingi kusoma mashairi. Ibun Ta'awidhi ametunga mashairi mazuri sana na marefu ya kuwasifia Watu wa Nyumba ya Mtume Mtukufu SAW.  Mashairi huyo kabla ya kupoteza macho yake alifanya jitihada kubwa za kukusanya athari zake na hata baada ya kupofuka macho yake aliendelea kutunga mashairi. Na miaka 498 iliyopita katika siku kama ya leo, kulitokea mapigano ya kihistoria ya Chaldoran kati ya Iran na dola la Othmania katika eneo la bonde lililoko kati ya Tabriz na Khoui, kaskazini magharibi mwa Iran. Mapigano hayo yalikuwa kati ya wapiganaji wa Shah Ismail Swafawi na vikosi vya Sultan Salim Othmani.  
 

No comments:

Post a Comment