TRANSLATE THIS BLOG

Friday, August 17, 2012


NAIBU MRATIBU WA SKAUTI TANGA;

JAMII YA KISLAM IZINGATIE MAFUNDISHO WALIYOPATA KATIKA KIPINDI HIKI

Huku zikiwa zimebakia siku chache kukamilika kwa mwezi wa ramadhani, Jamii ya kiislam imeaswa kuzingatia mafunzo  yatokanayo na mwezi  huo katika maisha yao ya kila siku.

Hayo yamesemwa na mratibu msaidizi wa skauti wa kiislamu mkoa wa Tanga Ustadh Selemani Amiri Mssey alipokuwa akitoa ujumbe wake katika ghafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na skauti wa kiislamu jiji la Tanga leo katika shule ya msingi Mwakidila.

Aidha aliwataka wazazi na walezi  kuhakikisha vijana wao wanasherehekea siku kuu ya Idd ul Fitr kwa kufuata mafunzo ya Mtume Mohammad (Swallalahu alaihi Wassallam) kwa kujiepusha na vitendo viovu.

Wengine waliohudhuria ni pamoja na kiongozi wa mafunzo ya gwaride la skauti jiji la Tanga kamanda Hassan Shakha pamoja na viongozi mbalimbali wa dini ya kiislamu jiji laTanga

No comments:

Post a Comment