TRANSLATE THIS BLOG

Monday, October 8, 2012




Timu ya utabibu ya Real Madrid imemnyooshea Cristiano Ronaldo alama ya kijani kwenda Ureno kuripoti kwa ajili ya majukumu ya kimataifa.

Mshambuliaji huyo hatari alikuwa katika maumivu ya bega katika mchezo huo wa jana wa ligi kuu ya soka nchini Hispania La Liga ambapo Madrid ilikwenda sare ya mabao 2-2 na Barcelona mchezo uliopigwa katika dimba la Nou Camp.

Kama hiyo haitoshi , Ronaldo tangu jana usiku amekuwa akifanyiwa uangalizi na madaktari wa Madrid akiwa nyumbani, na tayari mabingwa hao wa ligi ya Hispania wametangaza kupitia mtandao wa klabu hiyo kuwa Ronaldo hajapatwa na maumivu makubwa.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alitazamiwa kuelekea nyumbani Ureno mchana wa leo kwa ajili ya jukumu la kimataifa ambapo Ureno inatarajia kucheza dhidi ya Russia ijumaa mchezo wa kuwania tiketi ya kucheza fainali ya kombe la dunia 2014 kabla ya mchezo mwingine dhidi ya Ireland ya Kaskazini siku nne baadaye.
-----------------------------------------------------------

Kiungo wa Manchester City Barry: Siko tayari kustaafu soka la kimataifa

Kiungo wa Manchester City Gareth Barry amesisitiza kuwa hayuko tayari kustaafu soka la kimataifa huku  akiwa na matumaini makubwa kuwa atachaguliwa katika kikosi kitakacho tangazwa hivi karibuni, licha ya kutokuwepo katika kikosi kilichopita ambacho kilicheza dhidi ya San Marino and Poland.

Barry, ambaye alifanya kazi kubwa katika timu yake ya City ambayo ilichomoza na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Sunderland jumamosi, hajachaguliwa tangu mchezo wa kwanza wa kirafiki wa kocha Roy Hodgson dhidi ya Norway mwezi May.

No comments:

Post a Comment