TRANSLATE THIS BLOG

Friday, October 5, 2012


CAF yatangaza majina 34

Shirikisho la kandanda barani Afrika, CAF, limetoa orodha ya wachezaji 34 ambao watawania tuzo ya mchezaji bora zaidi wa soka katika bara hilo mwaka 2012.

Kati ya wachezaji hao, ni mchezaji Yaya Toure, kutoka Ivory Coast, na ambaye huichezea klabu ya Uingereza ya Manchester City.

Toure alitangazwa mshindi wa tuzo hiyo mwaka uliopita.
Katika orodha hiyo, wamo wachezaji watatu ambao huvichezea vilabu vya Afrika.
Wachezaji wawili wa Zambia, Rainford Kalaba na Stoppila Sunzu, wote ni wachezaji wa klabu ya TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, na Youssef Msakni kutoka Tunisia ni mchezaji wa Esperance.
Msakni hata hivyo anatazamiwa kuihama Esperance, na kuelekea Qatar mwezi Januari mwaka ujao, kujiunga na klabu ya Lekhwiya.
Kalaba na Sunzu tayari wana sifa za kutosha, baada ya kuwa miongoni mwa wachezaji walioiwezesha Zambia kuibuka mabingwa katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka huu nchini Gabon.


The GLO-CAF Awards Gala 2012  Itafanyika  Accra,Inchini  Ghana katika  Banquet Hall, State House  itakuwa ni mwezi  December 20th.

The other categories for which winners will be announced on Awards Gala are as following:

              1.       National Team of the Year
                      2.       Women’s Footballer of the Year
                            3.       Women’s National Team of the Year
4.       Club of the Year
                         5.       Most Promising Talent of the Year
 6.       Coach of the Year
   7.       Referee of the Year
8.       Legend Award
  9.       Fair Play Award
10.   Platinum Award
11.   Africa Finest XI





No comments:

Post a Comment