Kura za uchaguzi wa Angola zahisabiwa
Kura zinahisabiwa baada ya uchaguzi mkuu nchini Angola.
Huu ni uchaguzi wa pili tangu kumalizika kwa vita virefu vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Hata hivo kulikuwa na malalamiko kwamba kumetokea ulalamishi, huku baadhi ya wapigaji kura walikataliwa kura kwa sababu majina yao hayakuwemo kwenye daftari.
Rais Jose Eduardo dos Santos - ambaye amekuwa madarakani kwa zaidi ya miaka 30 - anataraji chama chake kitashinda na hivo kumpa yeye muhula mwengine wa uongozi
No comments:
Post a Comment