TRANSLATE THIS BLOG

Tuesday, September 18, 2012

UEFA CHAMPIONZ LIGI: Tathmini Mechi za leo Jumanne!



BIGI MECHI ni Santiago Bernabeu Real Madrid v Man City!!.....


UEFA_CHAMPS_LIGI

Jumanne ya leo Septemba 18 ndio mwanzo rasmi wa Michuano 

ya hatua ya Makundi ya UEFA ya kusaka Klabu Bingwa Ulaya, 

UEFA CHAMPIONZ LIGI, na zitakuwepo Mechi 8 za Makundi A

 hadi D lakini, bila shaka, kati ya hizo, BIGI MECHI, ile

 Mechi ya Mvuto, ni ile itakayochezwa Uwanja wa Santiago 

Bernabeu kati ya Mabingwa wa Spain Real Madrid na Mabingwa 

wa England, Manchester City.

=====================

RATIBA:

[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, TANZANIA]

Jumanne Septemba 18

GNK Dinamo - FC Porto

Paris Saint-Germain FC - FC Dynamo Kyiv

Montpellier Hérault SC - Arsenal FC

Olympiacos FC - FC Schalke 04

Málaga CF - FC Zenit St. Petersburg

AC Milan - RSC Anderlecht

Borussia Dortmund - AFC Ajax

Real Madrid CF - Manchester City FC

=====================

TATHMINI MECHI ZA JUMANNE

KUNDI A

-GNK Dinamo Zagreb v FC Porto

-Paris Saint-Germain FC v FC Dynamo Kyiv

=====================

Klabu ‘Tajiri’ Paris Saint-Germain wanarejea tena kwenye

 UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa mara ya kwanza tangu Msimu

 wa 2004/5 na watakuwa wenyeji wa Dynamo Kiev 

Uwanjani Parc des Princes.

PSG, chini ya Meneja Carlo Ancelotti, wameanza vyema 

kwenye Ligi ya Ufaransa, Ligi 1, kwa kutoka sare Mechi 3 na 

kushinda mbili huku Straika wao mkubwa Zlatan

 Ibrahimovich akipiga bao 5.

Mbali ya Ibrahimovich, PSG wanao hatari nyingine kina 

Javier Pastore na Ezequiel Lavezzi na pia kuanza tena 

kucheza kwa Beki toka Brazil, Thiago Silva, ambae hajaichezea 

Timu yake mpya baada ya kuumia akiwa na Brazil 

kwenye Michezo ya Olimpiki, kutawaongezea nguvu.

Lakini Dynano Kiev sio nyanya na wameanza vyema 

kwenye Ligi yao ya Ukraine kwa kupoteza Mechi mbili 

tu kati ya 9 walizocheza huku tishio lao kubwa likitoka 

kwa Mnigeria Ideye Brown ambae amewafungia 

bao 8 Msimu huu.

Kwenye Kiungo, Dynamo Kiev wanae Mchezaji wa zamani

 wa Tottenham Niko Kranjcar ambae kwenye Ligi ya 

Ukraine amepachika bao 4.

Mechi nyingine ya Kundi A ni ile itayochezwa Stadion Maksimir

 kati ya wenyeji Dinamo Zagreb na FC Porto.

Wakiwa bila ya Straika wao mahiri kutoka Brazil, Hulk, ambae 

wamemuuza kwa Zenit St Petersburg, FC  Porto 

watawategemea Lucho Gonzalez na James Rodriguez

 kuwapatia magoli.

Lakini Dinamo Zagreb, wakiwa na mashine yao ya Kibrazil 

ya magoli, Sammir, hawajafungwa hata Mechi moja

 kwenye Ligi yao Msimu huu, wapo kileleni, na 

watataka kufuta uchungu wa Msimu uliopita ambao

 kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI walifungwa Mechi zao

 zote 6 za Kundi lao na kupachikwa jumla ya bao 22.

Moja ya vipigo hivyo 6 ni kile cha 7-1 mikononi 

mwa Lyon na kuleta uzushi kuwa wamepanga matokeo.

KUNDI B

-Montpellier Hérault SC v Arsenal FC

-Olympiacos FC v FC Schalke 04

=====================

Straika wa Arsenal, Olivier Giroud, anarudi tena Klabu 

yake ya zamani Montpellier ambayo ilimuuza kwa 

Arsenal kabla Msimu huu kuanza huku akiwa bado 

akisaka bao lake la kwanza kwa Klabu yake 

mpya katika Mashindano rasmi.

Arsenal wanatinga kwenye Mechi hii ya Ulaya wakitoka

 kuitandika Southampton bao 6-1 hapo juzi mechi 

ambayo walicheza bila ya Giroud ingawa 

Mchezaji wao mpya mwingine, Lukas Podolski, aling’ara.

Tofauti na Arsenal, Mabingwa wa Ufaransa

 Montpellier wanatinga kwenye Mechi hii wakiwa 

wanasuasua huko kwao kwenye Ligi 1 wakiwa 

wameshinda Mechi moja tu kati ya 5 walizocheza

 ikiwa ni pamoja na kichapo cha 3-1 mikononi 

mwa Reims Ijumaa iliyopita.

Katika Mechi nyingine ya Kundi B, Schalke watakuwa

 safarini kucheza Uwanja wa Karaiskakis nyumbani 

kwa Mabingwa wa Ugiriki Olympiacos ambao 

wameanza vyema kutetea Taji lao kwa 

kushinda Mechi zao zote 3.

Tishio kubwa kwa Olympiacos ni toka kwa Schalke

 ni lile la Straika wa Holland Klaas-Jan Huntelaar

 ambae ni mfungaji hatari.

KUNDI C

-Málaga CF v FC Zenit St Petersburg

-AC Milan v RSC Anderlecht

=====================

AC Milan, walioanza vibaya kwenye Ligi yao ya Italy

 Serie A na pia kuchapwa 1-0 hivi juzi na Atalanta,

 wanawakaribisha Timu ngumu ya Anderlecht ya 

Ubelgiji ambayo huko kwao haijafungwa katika Mechi 7.

Chini ya Kocha Massimiliano Allegri, AC Milan bado

 inayumbishwa na kuondokewa kwa Nyota wao

 kadhaa Msimu huu ambao ni Zlatan Ibrahimovic

 na Thiago Motta waliokwenda Paris Saint-Germain

 na wengine ni Wakongwe Alessandro Nesta, 

Filippo Inzaghi, Gianluca Zambrotta, Gennaro Gattuso,

 Mark van Bommel na Clarence Seedorf.

Pia AC Milan imempoteza Straika Antonio Cassano 

ambae walibadilishana na yule wa Inter Milan 

Giampaolo Pazzini lakini pia wameweza kununua 

Wachezaji wawili, Kiungo Nigel de Jong 

na Beki Francesco Acerbi.

Mechi nyingine ya Kundi C ni kati ya Timu mbili ambazo

 zimeanza vizuri Ligi za nyumbani kwao ambazo ni 

Malaga ya Spain na Zenit St Petersburg ya Urusi.

Ingawa Malaga wamempoteza Santi Cazorla 

alieenda Arsenal lakini kwenye La Liga 

wanafanya vyema na wako nafasi ya pili.

Zenit St Petersburg, chini ya Kocha Luciano Spalletti,

 wanafanya vyema hasa ukuta wao imara na

 Straika Alexander Kerzhakov amekuwa akifunga 

bao zao nyingi kabla na kuimarishwa kwa 

kuwanunua Hulk na Kiungo Axel Witsel.

KUNDI D

-Borussia Dortmund v AFC Ajax

-Real Madrid CF v Manchester City FC

=====================

Mechi ya Real Madrid na Manchester City Uwanjani

 Santiago Bernabeu ndio gumzo la kila pembe Duniani.

Man City, chini ya Kocha Roberto Mancini, Msimu 

uliokwisha walishindwa kuvuka hatua ya Makundi

 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na safari hii tena wako

 kwenye ‘Kundi la Kifo’ ambalo pia wako Mabingwa

 wa Ujerumani Borussia Dortmund na Mabingwa 

wa Holland, Ajax Amsterdam.

Hii ndio Mechi ambayo, pengine, itathibitisha 

kukomaa kwa Man City lakini pengine imekuja 

kwao kwenye wakati mbaya kwani Real Madrid,

 chini ya Kocha makeke Jose Mourinho, wako 

kwenye wakati mgumu kwenye La Liga baada ya 

kuanza utetezi mbovu wa Taji lao huko Spain.

Wakati Man City hawajafungwa kwenye Ligi Kuu 

England wakiwa nafasi ya 4, Real Madrid wameshinda

 Mechi moja tu na wapo nafasi ya 14 kwenye La Liga

 huku wakigubikwa na utata kuhusu hatima ya Staa

 wao mkubwa Cristiano Ronaldo ambae amebainisha

 hana furaha Klabuni hapo.

Hii ni Mechi ambayo Mourinho lazima ashinde ili kurekebisha

 Jahazi lake linaloenda mrama na hilo, pengine, linaweza 

kuashiria maafa kwa Man City.

Mechi nyingine ya Kundi D ni ile itakayochezwa 

Westfalenstadion, Uwanja ambao unasifika kwa

 kelele, pale Ajax Amsterdam watakapotua kuwavaa

 wenyeji Borussia Dortmund.

Baada ya kumpoteza Shinji Kagawa aliehamia Manchester

 United, Dortmund walimnunua Marco Reus toka

 Borussia Moenchengladbach na amekuwa moto.

Lakini Ajax, chini ya Staa wa zamani wa Holland Frank de Boer

, si mzaha na Msimu huu hawajapoteza Mechi.

Ajax, licha ya kuwapoteza Wachezaji wao Jan Vertonghen

 (aliekwenda Tottenham), Gregory van der Wiel (Paris Saint-Germain)

 na Vurnon Anita (Newcastle United), bado wanao 

wengine tishio kina Thulani Serero, Tobias Sana na Siem de Jong.

RATIBA:

[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, Bongo Taimu]

Jumatano Septemba 19

FC Shakhtar Donetsk - FC Nordsjælland

Chelsea FC - Juventus

LOSC Lille - FC BATE Borisov

FC Bayern München - Valencia CF

FC Barcelona - FC Spartak Moskva

Celtic FC - SL Benfica

Manchester United FC - Galatasaray A.S.

SC Braga - CFR 1907 Clu

No comments:

Post a Comment