Arshavin aikataa Dinamo Moscow
Andrey Arshavin alikataa kujiunga na klabu ya Russia,Dinamo Moscow,siku ya mwisho ya dirisha la usajili kufungwa na kutaka kuendelea kusalia Emirates kupigania namba katika kikosi cha kwanza.

Arsenal walimpa Arshavin, 31,offer ya kujiunga kwa mkopo wa mwaka mmoja na Dinamo lakini tofauti na matarajio mrusi huyo alikataa.
Meneja wa Dinamo, Dan Petrescu amethibitisha maamuzi ya Arshavin: na kusema kuwa nilikuwa namuhitaji mchezaji huyo lakini Andrey akasema hapana kwa Dinamo."
Nahodha hhuyo wa Russia alipoteza nafasi yake katika kikosi cha kwanza Arsenal msimu uliopita na kucheza kwa mkopo katika klabu yake ya zamani ya Zenit St Petersburg.
Arsharvin katika msimu wote alikuwa akihusishwa na vilabu vya Russia ,Zenit na CSKA Moscow ambazo zilionyesha nia yakumuhitaji moja kwa moja…
Siku zilizopita , Arshavin alisema angependelea kurudi nyumbani na kuichezea klabu yake aipendayo ya Zenit.
No comments:
Post a Comment